HUYU NDIYE WAZIRI MKUU WA SERIKALI YA MAGUFULI; SOMA HAPA KUJUA WASIFU WAKE

KUJISHINDIA MAMILIONI KATIKA DROO HII BONYEZA HAPA CHINI UJIUNGE KATIKA BAHATI NASIBU,NA ILI UIBUKE MSHINDI HAKIKISHA KILA SIKU WABONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA;
Hatimaye kazi ya kutambua jina la waziri mkuu ajaye imekuwa rahisi zaidi baada ya majina ya watu wanaotajwa kuwa ndiyo walio mbioni kuteuliwa na Rais Dk. John Magufuli kushika nafasi hiyo kupungua hadi kubakia sita.

Taarifa za uhakika ambazo Nipashe imezipata zimebainisha kuwa hivi sasa, majina yaliyo na nafasi kubwa ya kuwa miongoni mwa wale watakaotajwa na Rais Magufuli ni pamoja na Mbunge wa Ruangwa mkoani Lindi, Kassim Majaliwa na pia Jenista Mhagama wa Jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma.
 

Chanzo hicho kimefichua kuwa wabunge wengine wanne walio katika orodha itakayotoa jina la Waziri Mkuu ni Mbunge wa Bagamoyo aliyekuwa Waziri wa Elimu, Dk. Shukuru Kawambwa; Mbunge wa Chemba aliyekuwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia; Mbunge wa Mtwara Vijijini aliyekuwa Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Hawa Ghasia na Mbunge wa Jimbo la Newala aliyekuwa Waziri katika Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Kapt. George Mkuchika.

Chanzo kimeihakikishia Nipashe kuwa katika orodha hiyo ya wabunge sita, mmoja wao atakuwa Waziri Mkuu na wengi wataduwazwa kwani siyo miongoni mwa wale maarufu wanaotajwatajwa kwa zaidi ya wiki moja sasa.

Hadi sasa, majina ambayo yamekuwa yakitajwa mara kwa mara na taarifa zao kusambazwa kwenye mitandao mingi ya kijamii ni pamoja na Mbunge wa Jimbo la Isimani (Iringa), William Lukuvi; Mbunge wa Iramba Magharibi (Singida), Mwigulu Nchemba; Mbunge wa Bumbuli (Tanga), January Makamba; Mbunge wa Jimbo la Kyela (Mbeya), Dk. Harrison Mwakyembe, Mbunge wa Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo; Mbunge wa Iramba Mashariki (Singida), Lazaro Nyalandu na pia Mbunge wa Tunduru Kaskazini, Mhandisi Ramo Makani.

Ratiba iliyotolewa wiki iliyopita ilionyesha kuwa Rais Magufuli atawasilisha jina la waziri mkuu wa serikali yake keshokutwa ili wabunge wapate nafasi ya kumpigia kura (waziri mkuu huyo) na kisha kufuatia shughuli ya kuzindua rasmi Bunge hilo la 11.

Chanzo kiliiambia Nipashe kuwa jina hilo la waziri mkuu linafahamika na tayari kuna harakati kadhaa zimeanza kuchukuliwa kuhakikisha kuwa kila kitu kinakwenda vizuri.
“Kinachosubiriwa sasa ni kwa Spika wa Bunge kupelekewa jina hilo tu… hakuna mwenye ujasiri wa kulitaja wazi kwani mwenye jukumu hilo ni rais mwenyewe,” chanzo kiliiambia Nipashe.

Hata hivyo, chanzo hicho kiliainisha sifa kadhaa muhimu ambazo ndizo zimeipa Nipashe ujasiri wa kutambua kuwa waziri mkuu ajaye ni kati ya majina sita, yakiwamo ya Jenista na Majaliwa.

KWA NINI NI KINA MAJALIWA?
Sifa hizo muhimu za mtu atakayetambulishwa bungeni kuwa ndiye waziri mkuu, kwa mujibu wa chanzo chetu, ni pamoja na mahala atokako. Kwamba, yeye hatoki katika mikoa ya kanda za magharibi, ziwa wala kaskazini.

Sifa ya pili ya mtu huyo ni kutowahi kujitokeza katika mbio za kuwania urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi.
“Sifa muhimu ya tatu kwa mtu huyu ni kwamba, hajawahi kudhaniwa kushika nafasi hiyo na hivyo, atakapotajwa bungeni watu wengi wataduwazwa,” chanzo kilieleza.

Kadhalika, sifa ya nne ya mtu huyo atakayetajwa kushika nafasi hiyo ya uwaziri mkuu ni kwamba, amewahi kushikilia nafasi ya uwaziri/naibu waziri katika serikali ya awamu ya nne ya Rais Jakaya Kikwete iliyomaliza muda wake Novemba 5, 2015.

“Naye alikuwamo katika kundi la mawaziri na manaibu waziri waliomaliza na Rais Kikwete,” chanzo kilifafanua
Kwa kuzingatia sifa hizo, ndipo Nipashe ilipofanya uchunguzi binafsi na kubaini maijina sita ya wale wanaoendana na sifa hizo.

Kwanza, mikoa isiyokuwa ya ziwa, nyanda za juu na kaskazini ni ya Kanda ya Kati, ambayo ni Singida na Dodoma; Mashariki na Pwani ambayo ni Morogoro, Pwani na Dar es Salaam na pia mikoa ya Kusini ambayo ni Lindi, Mtwara na Ruvuma.

Aidha, wabunge wanaotoka kwenye mikoa hiyo huku wakiwa na sifa ya kuwamo katika orodha ya mawaziri wa mwisho wa Rais mstaafu Kikwete, wasiowahi kuwania urais na pia wanaowexza kushangaza wengi pindi mmoja wao akitajwa kuwa waziri mkuu ni Nkamia wa Chemba (Dodoma), Dki. Kawambwa wa Bagamoyo (Pwani), Majaliwa wa Ruangwa (Lindi), Ghasia wa Mtwara Vijini (Mtwara) na Jenista wa Peramiho (Ruvuma).

UTABIRI WA WABUNGE
Wakati chanzo cha Nipashe kikitaja sifa zinazowagusa kina Majaliwa, wabunge mbalimbali walioongea na Nipashe kwa sharti la kutotajwa majina yao wamesema ni vigumu kutabiri kwani Rais Mgufuli ni msiri na hadi sasa, kuna taarifa kuwa tayari ameshawatimua watu kadhaa waliojaribu kumuendea kwa nia ya kujipendekeza kwake ili awakumbuke au kupeleka majina ya watu wao. 


“Magufuli ni kiongozi tofauti sana… hakuwa na mtandao wowote uliomsaidia kuingia Ikulu na hivyo mambo mengi ni ya siri, hayavuji kirahisi,” mbunge mmoja wa CCM aliiambia Nipashe jana.

Mbunge mwingine alisema katika uteuzi wa mawaziri wakuu waliopita, ilikuwa rahisi kubashiri kwa sababu taarifa mbalimbali zilikuwa zikiwafikia kabla hata ya tangazo rasmi bungeni, lakini sasa hali ni tofauti.

"Hivi sasa wabunge wa CCM hatujui lolote ... safari hii Rais (Magufuli) amefanya siri na wengi hatujui kinachoendelea," alisema.
Hata hivyo, baadhi ya wabunge walieleza sifa za watu ambaoe wanatamani wapewe nafasi hiyo, huku wengine wakitaja majina ya William Lukuvi aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa anafaa, na wengine wakiwataja aliyekuwa Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, Mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo na Mbunge wa Muheza, Adadi Rajabu.

Mbunge wa Mtera, Livingstone Lisinde, alisema hawezi kutabiri jina, lakini angependa Waziri Mkuu awe ni mwanasiasa makini, mwadilifu na mwenye kuchukua hatua za haraka.

Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ali Kessy, alisema anatakiwa mfuatiliaji wa mambo ya kila siku, awe mkali na kwamba katika uendeshaji wa serikali, kamwe asibague watu, makundi na afanye kazi kwa matakwa ya kanuni, sheria na katiba ya nchi.

"Wananchi wamechoshwa na hatua ya serikali kuwahamisha watumishi wanaoharibu sehemu moja na kuwapeleka kwingine. Hivyo ni lazima Waziri Mkuu ajaye awe na sifa ya kuwachukulia hatua za kisheria watu wa aina hiyo na asiwaogope… hata kama kuna undugu na urafiki," alisema Kessy.
MATARAJIO WAZIRI MKUU WA MAGUFULI

Baada ya uteuzi wa Mwanasheria Mkuu alioufanya siku ya kuapishwa kwake (Alhamisi), Magufuli alisubiri saa chache tu kabla ya kutembea kwa miguu kutoka ofisini kwake hadi katika jingo la Wizara ya Fedha ambako alifanya ziara ya kustukiza, akiingia kila ofisi kuona shughuli za ujenzi wa taifa zinavyoendelea

Ni wazi kwamba kwa kufanya hivyo, Magufuli anaonyesha kuwa Waziri Mkuu wake atapaswa kuwa mtu wa vitendo zaidi na siyo maneno mengi.

Kadhalika, utoaji wa maamuzi kuanzia siku ya kwanza ni sifa muhimu ya kile alichokuwa akikisisitiza wakati wa kampeni kuwa kamwe, hatavumilia mawaziri wanaopenda majibu ya ‘tuko mbioni’, ‘tuko kwenye mchakato’, ‘tuko kwenye hatua nzuri’ wala ‘tuko kwenye hatua za mwisho’. Ni kazi tu.

Aidha, Magufuli ameshaoonyesha vilevile kuwa Waziri Mkuu wake atakuwa ni mtu wa kutoa maamuzi kwa kasi. Sifa hii inatokana na muda alioutumia katika kutangaza jina la Mwanasheria Mkuu na pia siku ya kuanza kwa Bunge la 11.

Magufuli pia ameshafanya kikao kizito na makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu, gavana wa Benki Kuu (BoT) na Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Katika kikao hicho, alitoa maelekezo kadhaa yaliyofichua sifa nyingine muhimu atakazokuwa nazo Waziri Mkuu wake na pia mawaziri wengine.

Rais Magufuli aliagiza pia kufutwa mara moja kwa safari za nje za mawaziri na viongozi wengine wa juu serikalini na kwenye taasisi za umma.

Aliagiza kuwa masuala yote ya nje ya nchi yatekelezwe na mabalozi waliopo huko na kwamba, kukiwa na ulazima, basi safari hizo ni lazima ziidhinishwe na yeye (Rais) au Katibu Mkuu Kiongozi, Ikulu. Rais Magufuli aliagiza kuwa anachotaka ni kuona viongozi wakifanya ziara nyingi kwa wananchi vijijini na kuwatatulia kero zao. Hii ni dalili nyingine ya wazi kuwa Waziri Mkuu ajaye hatakuwa mtu wa kusafiri nje mara kwa mara na badala yake, atakuwa ni mtu wa kuwa karibu na wananchi huku akisimamia shughuli za serikali kwa umakini zaidi.

Katika hili, ipo sifa nyingine anayotarajiwa kuwa nayo Waziri Mkuu mpya, ambayo ni kuwa na jicho la ziada kuhakikisha kuwa serikali haipati hasara kwa kuuziwa vitu kwa bei ya juu kuliko iliyopo sokoni.

Sifa nyingine muhimu kwa Waziri Mkuu ni kuwa mzoefu wa kukabili changamoto za hoja moto za wapinzani bunegni kwani katika Bunge lijalo, kambi ya upinzani itakuwa na wabunge 121. Kwa sababu hiyo, ni wazi kwamba mtu atakayeteuliwa na Rais Magufuli kwa nafasi ya Waziri Mkuu ni lazima atakuwa na sifa ya kukabiliana na maswali ya wabunge machachari wa upinzani pale inapobidi, ikiwamo wakati wa maswali ya papo kwa papo.

Kwa ujumla, kama ilivyowahi kuripotiwa katika gazeti hili, sifa muhimu za ujumla kwa Waziri Mkuu wa Magufuli zatarajiwa kuwa ni uadilifu, kwa maana ni lazima awe mtu asiyekuwa na chembe ya kashfa, hasa zinazohusiana na rushwa kama ilivyo kwa mwenyewe (Rais Magufuli); Kujiamini kiasi cha kutoa maamuzi magumu na kwa wakati kwa ajili ya maslahi ya taifa; kufanya kazi kwa pamoja na siyo kusaka umaarufu binafsi kiasi cha kumpiku Rais; Uwezo wa kusimamia utekelezaji wa mipango ya serikali na pia Kukubalika ndani na nje ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
CHANZO: NIPASHE
KUJIUNGA NA KINYANG'ANYIRO CHA PIKIPIKI AINA YA BOXER BONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA NA UIBUKE MSHINDI,BONYEZA MARA NYINGI UWEZAVYO KUIBUKA MSHINDI;

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UDAKU WA DUNIA Published.. Blogger Templates
Back To Top