Manchester United wamekuwa wakikosolewa sana juu ya sera yao ya usajili katika kipindi miaka kadhaa sasa, hasa chini ya utawala wa Louis van Gaal na Ed Woodward. Man United imetumia zaidi ya robo billioni ya paundi za kiingereza tangu LVG alipoanza kazi June 2014. Inaonekana wazi linapokuja suala la usajili klabu hiyo inakosa uzoefu wa namna ya kudili la usajili tangu Ed Woodward alipomrithi David Gill.
Ed Woodward amefanya kazi nzuri katika upande wa masoko/biashara na anastahili sifa, lakini kazi nyingine pia ni kupata dili zenye kuinufaisha klabu, jambo ambalo amelimudu kwenye biashara za matangazo/udhamini kwa mfano dili za Adidas na Chevrolet. Adidas watailipa Man United €750m kwa miaka 10 na Chevrolet watalipa kiasi cha €350M kwa muda wa miaka 7..
Linapokuja suala la uhamisho wa wachezaji, Woodward bado anaonekana kutokufanya vizuri – mfano ukiangalia uhamisho aa Maroune Fellaini kutoka Everton kwenda United – Man United walilipq £4m zaidi ya ilivyotakiwa katika kipengele cha kuvunja mkataba wa Fellaini na Toffes na pia alifeli katika usajili wa Pedro kutoka Barcelona baada ya kuzidiwa kasi na Chelsea. United pia walimsajili Anthony Martial kwa £36m na inaweza kufika zaidi ya £50m ikiwa atapata mafanikio na klabu hiyo, hili liliwafanya watu/wachambuzi wa soka kuanza kuwa na mashaka na utendaji wa United kwenye suala la uhamisho wa wachezaji na je kama wana mipango endelevu ya mbeleni.
Tangu Sir Alex Ferguson alipostaafu, Man United wamekuwa katika kipindi cha mpito wa mabadiliko na kipindi hiki kitaendelea mpaka Louis Van Gaal atakapoondoka mkataba wake utakapoisha 2017. Louis Van Gaal kwasasa hasumbuliwi na mafanikio ya muda mfupi, naamini maono yake yanatoa majawabu endelevu ya kipindi cha mbele na anatengeneza msingi mzuri kwa kocha ajaye wa Manchester United.
WACHEZAJI WALIOUZWA NA UNITED CHINI YA LVG
Sera ya Louis Van Gaal katika kuijenga United itakayodumu kwa kipindi kirefu inaweza kuonekana katika madirisha mawili ya usajili ya mwaka 2014 na 2015. Wakati vipindi hivi viwili vya usajili – Van Gaal amewauza wachezaji wa kikosi cha kwanza 13 ambao umri wao ulikuwa si chini ya miaka 27 na wachezaji wengine ambao hawakuwa wanafiti kuendelea kuitumikia klabu, wachezaji aina ya akina Nani, Anderson, Welbeck, Cleverley, Evans na hata Angel Di Maria (aliyetaka kuondoka mwenyewe). Kama Louis Van Gaal angewaacha wachezaji hawa klabuni basi wangeuzwa msimu ujao au wa baada hivyo uamuzi wa kuwauza ndani ya miaka vipindi viwili vilivyopita vya usajili ulikuwa sahihi kwa sababu United imewauza wakiwa bado na thamani katika soko la usajili. Kama angewaacha wangeendelea kuwa mzigo wa ziaa usioendana na mahitaji ya timu kwa kocha ajaye – na labda isingepatikana wigo mpana wa kusajili wa wachezaji wapya.
Sera ya Louis Van Gaal katika kuijenga United itakayodumu kwa kipindi kirefu inaweza kuonekana katika madirisha mawili ya usajili ya mwaka 2014 na 2015. Wakati vipindi hivi viwili vya usajili – Van Gaal amewauza wachezaji wa kikosi cha kwanza 13 ambao umri wao ulikuwa si chini ya miaka 27 na wachezaji wengine ambao hawakuwa wanafiti kuendelea kuitumikia klabu, wachezaji aina ya akina Nani, Anderson, Welbeck, Cleverley, Evans na hata Angel Di Maria (aliyetaka kuondoka mwenyewe). Kama Louis Van Gaal angewaacha wachezaji hawa klabuni basi wangeuzwa msimu ujao au wa baada hivyo uamuzi wa kuwauza ndani ya miaka vipindi viwili vilivyopita vya usajili ulikuwa sahihi kwa sababu United imewauza wakiwa bado na thamani katika soko la usajili. Kama angewaacha wangeendelea kuwa mzigo wa ziaa usioendana na mahitaji ya timu kwa kocha ajaye – na labda isingepatikana wigo mpana wa kusajili wa wachezaji wapya.
Louis Van Gaal amefanya usajili wa wachezaji wenye umri mdogo ambao uwezo/nafasi kubwa katika ujenzi mpya wa timu. Katika utawala wa LVG, Man United imesajili wachezaji 8 wa kikosi cha kwanza ambao wana umri chini ya miaka 25, wachezaji kama Memphis, Matteo Darmian, Anthony Martial, Morgan Schneiderlin Luke Shaw, Marcos Rojo na Daley blind, waongeze na hawa Chris Smalling, Phil Jones, Paddy McNair, Andreas Pereira, Jesse Lingard, Adnan Januzaj na James Wilson ambao wote walikuwa chini ya umri wa miaka 25, hivyo wakati Louis Van Gaal atakapoondoka, kocha ajaye atakuwa na kundi la wachezaji ambao ndio watakuwa wanaingia katika awamu bora ya wanasoka kiumri – jambo linalotoa picha nzuri ya mbeleni kwa Man United. Ni muhimu kwa kocha ajaye wa United kuwa misingi mizuri ambayo itamuwezesha kufanikiwa Old Trafford. Naamini mipango ya LvG ni kuwekeza kwa ajili ya siku za usoni, anatengeneza mazingira mazuri ya kazi kwa atakayemrithi ili waiondoe Ujited katika kipindi cha mpito wa mabadiliko na kurudi katika zama kushindana/kutwaa makombe mbalimbali kama ilivyozoeleka.
Louis Van Gaal ana filosofi na uwezo mkubwa wa kukuza vipaji vichanga na kuhakikisha wachezaji wanakuwa bora kama ambavyo alivyoweza kufanya hayo akiwa na Ajax, Barcelona na Bayern Munich – hivyo anaamini anaweza kufanikiwa tena akiwa na United yenye wachezaji wenye umri mdogo na vipaji, wakiwaangalia Chris Smalling na Luke Shaw wameboreka zaidi chini ya uangalizi wa LvG. Japokuwa United walijaribu na kufeli kusajili wachezaji wa daraja la dunia katika maeneo yaliyokuwa na uhitaji – lakini waliweza kumsajili Bastian Schweinsteiger ambaye atamrithi Carrick kama kiungo mzoefu katika kikosi wakati Carrick atakapoondoka, Bastian ni mdogo wa miaka miwili kwa Carrick na atakuwepo United labda mpaka kocha mpya atakapokuja. Picha ya hapo juu inaonesha umri wa wachezaji wa sasa katika kipindi cha miaka mwili ijayo na unaweza kuona ishara nzuri, kutakuwepo na na wachezaji wachanga chini ya umri wa miaka 23na wachezaji wengine ambao watakuwa wanaingia katika umri wa viwango vya kuboreka zaidi -hivyo utakuwepo mchanganyiko mzuri wa wachezaji wachanga na wenye uzoefu – hili litampa misingi mziuri ya utendaji kocha ajaye wa United.
Filed Under:
EPL,
INTERNATIONAL NEWS,
SPORTS,
TRANSFERS
on Tuesday, September 29, 2015
Post a Comment