Waziri Mkuu Majaliwa Afanya Ziara ya Kushtukiza Bandarini.....Awafuta Kazi na Kuamuru Kukamatwa Kwa Maofisa Kibao wa TRA

KUJISHINDIA MAMILIONI KATIKA DROO HII BONYEZA HAPA CHINI UJIUNGE KATIKA BAHATI NASIBU,NA ILI UIBUKE MSHINDI HAKIKISHA KILA SIKU WABONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA;

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amefanya ziara ya kushtukiza katika Bandari ya Dar es Salaam mapema leo na kubaini upotevu wa makontena 349.

 Waziri Mkuu amebaini upotevu wa makontena hayo ambayo yana thamani ya zaidi ya shilling bilioni 80, na kuagiza kufutwa kazi mara moja kwa maafisa waliohusika na upotevu huo.

Majaliwa amewasimamisha kazi Kamishna wa Kodi, Tiagi Masamaki pamona na Habibu Mpozya wa kitengo cha huduma kwa wateja.

Uamuzi huo wa Waziri Mkuu umekuja baada ya kubaini kuwa katika kumbukumbu za Mamlaka ya Bandari kuna taarifa ya makontena 349 yenye thamani ya shilingi bilioni 80 lakini taarifa hizo hazipo kwenye kumbukumbu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Waziri Mkuu ameelekeza Polisi kuwakamata maafisa wote waliohusika na sakata hilo kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

KUJIUNGA NA KINYANG'ANYIRO CHA PIKIPIKI AINA YA BOXER BONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA NA UIBUKE MSHINDI,BONYEZA MARA NYINGI UWEZAVYO KUIBUKA MSHINDI;

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UDAKU WA DUNIA Published.. Blogger Templates
Back To Top