Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa Kushtakiwa FIFA kwa kauli hii......

KUJISHINDIA MAMILIONI KATIKA DROO HII BONYEZA HAPA CHINI UJIUNGE KATIKA BAHATI NASIBU,NA ILI UIBUKE MSHINDI HAKIKISHA KILA SIKU WABONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA;

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa.

MWENYEKITI wa Chama cha Wanasoka wa Algeria, Ahmed Boudry ameamua kumfungulia mashitaka Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa. 
Boudry amesema wamekerwa kupita kiasi na kauli ya Mkwasa kwamba raia wa Algeria ni wabaguzi wakubwa wa rangi, hivyo amemfungulia mashitaka Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa). 

“Alisema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari hata kabla ya mechi ambayo Tanzania ilifungwa bao saba. Tunaamua kumfikisha Fifa kwa kuwa amewadhalilisha raia wote wa Algeria wakiwemo wachezaji. 
“Hakuwa na ushahidi, Tanzania imekuja hapa zaidi ya mara moja na hatujawahi kupata malalamiko ya ubaguzi wa rangi, vipi yeye Mkwasa aseme hayo?” alihoji kiongozi huyo. 

Kabla ya kauli yake hiyo, vyombo vingi vya habari vya Algeria vilizungumzia suala la Mkwasa kusema Waalgeria ni wabaguzi wa rangi. Vyombo hivyo vya habari vya Algeria ikiwemo mitandao inayotumia lugha ya Kifaransa vilimshambuliaji Mkwasa kwa madai amewakashifu Waalgeria. 

Algeria iliing’oa Stars kwa kuifunga mabao 7-0 katika mechi ya marudiano mjini Blida ambayo ilikuwa ya kufuzu Kombe la Dunia 2018. Stars imeaga michuano hiyo kwa kufungwa jumla ya mabao 9-2 kwani awali ilitoka sare ya mabao 2-2 jijini Dar es Salaam kwenye Uwanja wa Taifa.

KUJIUNGA NA KINYANG'ANYIRO CHA PIKIPIKI AINA YA BOXER BONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA NA UIBUKE MSHINDI,BONYEZA MARA NYINGI UWEZAVYO KUIBUKA MSHINDI;

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UDAKU WA DUNIA Published.. Blogger Templates
Back To Top