ANAYETAKA USPIKA WA BUNGE LA TANZANIA RUKSA - CCM

KUJISHINDIA MAMILIONI KATIKA DROO HII BONYEZA HAPA CHINI UJIUNGE KATIKA BAHATI NASIBU,NA ILI UIBUKE MSHINDI HAKIKISHA KILA SIKU WABONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA;


Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dar es Salaam. Wakati makada wa CCM, wakionyesha nia ya ‘kimya kimya’ kuwania nafasi ya kiti cha Spika wa Bunge la 11, chama hicho kimesema anayetaka nafasi hiyo ruksa kujipitisha kwa wabunge kuomba kura.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Idara ya Oganaizesheni, Dk Muhammed Seif Khatibu alisema jana kuwa wanachama wake wanao uhuru wa kufanya maandalizi yao ya kujitangaza. “Sisi bado hatujaanza rasmi lakini hatuwezi kuwazuia wanachama wanaotaka nafasi hiyo kuanza kufanya ‘lobbying’ mapema... ni haki yao,” alisema.
Khatibu alisema CCM kwa sasa hawajaanza kutoa fomu za kuwania nafasi hiyo kwa wagombea wake hadi ofisi ya Bunge itakapotangaza rasmi kuwania nafasi hiyo.
“Tunasubiri ofisi ya Spika wa Bunge watangaze kwanza utaratibu wao na sisi ndiyo tutaanza kutoa fomu hizo na siwezi kusema itakuwa lini,” alisema Dk Khatibu.
Hadi sasa makada wanaotajwa kuwania nafasi hiyo ni Samuel Sitta na Anne Makinda, waliokalia kiti cha spika wa mabunge mawili yaliyopita.
Wengine wanaotajwa kuwania kiti hicho, wabunge wateule, Mussa Hassan Zungu (Ilala), Jenista Mhagama (Peramiho), George Simbachawene (Kibakwe) na Job Ndugai (Kongwa).
Kikatiba, kiti cha spika kinaweza kuwaniwa na mtu yeyote ambaye atapitishwa na chama chake bila ya kujali kama ni mbunge.
Iwapo mgombea hatakuwa mbunge mteule, ni lazima jina lake lipitishwe na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Wakati hali ikiwa haijapamba moto ndani ya CCM, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu jana alisema vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambavyo ni Chadema, NCCR-Mageuzi, NLD na CUF havijaanza mikakati ya kupitisha mtu atakayegombea uspika, badala yake vinaandaa kambi imara ya upinzani kwa ajili ya kuibana Serikali bungeni.
Akizungumzia utaratibu wa kumpata spika, Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, John Joel aliliambia gazeti hili hivi karibuni kuwa wagombea wa nafasi hiyo wanaruhusiwa kutoka vyama mbalimbali vya siasa.
Joel alisema mchakato wa kuwania nafasi hiyo utaanza baada ya Rais John Magufuli kuitisha Bunge.
“Nafasi hii haigombewi na mgombea binafsi. Ni lazima apitishwe na chama. Kama ni mbunge mteule jina lake linaletwa moja kwa moja katika ofisi za Bunge ila kama ni mwanachama wa kawaida lazima athibitishwe na NEC kuona kama ana sifa,” alisema Joel.
Alisema Rais akishaitisha vikao vya Bunge, chombo hicho cha kutunga sheria ndiyo kitaanza mchakato wa uchaguzi wa spika na kazi ya kwanza itakuwa kupokea majina ya wagombea kutoka vyama mbalimbali.
KUJIUNGA NA KINYANG'ANYIRO CHA PIKIPIKI AINA YA BOXER BONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA NA UIBUKE MSHINDI,BONYEZA MARA NYINGI UWEZAVYO KUIBUKA MSHINDI;

Post a Comment

CodeNirvana
Newer Posts Older Posts
© Copyright UDAKU WA DUNIA Published.. Blogger Templates
Back To Top