KUJISHINDIA MAMILIONI KATIKA DROO HII BONYEZA HAPA CHINI UJIUNGE KATIKA BAHATI NASIBU,NA ILI UIBUKE MSHINDI HAKIKISHA KILA SIKU WABONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA;
Juma Sufiani, Daktari wa timu ya Yanga
Kufuatia kuumia (kuvunjika mifupa miwili ya mguu wa kulia) kwa mchezaji Luke Shaw wa Manchester United wakati timu yake ikicheza mchezo wa michuano ya UEFA Champions League dhidi ya PSV, mtandao huu ulimtafuta daktari wa timu ya Yanga Juma Sufiani ili kutaka kujua mambo kadhaa kuhusiana na jeraha alilopata Shaw.
Dkt. Sufiani ameeleza mambo kadhaa ambayo ni ya kitaalamu zaidi wakati akifanya mahojiano mafupi mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa ligi kuu Tanzania bara kati ya Yanga dhidi ya Tanzania Prisons uliopigwa jana kwenye uwanja wa Taifa.
Shaffihdauda.com: Mchezaji wa Manchester United Luke Shaw amevunjika mguu (multiple fracture) hii kitaalamu ikoje?
Juma Sufiani: Huwa inatokea, mtu anaweza kuvunjiaka hata mara tatu lakini mara nyingi ‘multiple fracture’ huwa inatokea kwenye mifupa ya mbavu mara chache hutokea kama hivyo kwenye mifupa ya miguuni, na inapotokea inatibika kabisa na mtu anapona.
Shaffihdauda.com: Tatizo kama hili linaweza kuchua hadi muda gani ili mtu kupona kabisa na kurejea katika hali yake ya kawaida?
Juma Sufiani: Kupona inategemea mtu na mtu, wakati mtu mmoja atachukua muda flani mwingine inaweza ikachukua muda mrefu zaidi itategemea na jinsi alivyotibiwa.
Shaffihdauda.com: Na ‘alternatives’ zake zikoje anaweza akawekewa kitu gani mguuni kati ya chuma au Plaster of Paris (P.O.P)?
Juma Sufiani: Madactari watakavyoona, anaweza akawekewa chuma au P.O.P kutegemea na seriousness ya tatizo, inawezekana ikawa karibukaribu isiunge vizuri au ikawa mbali ikaunga vizuri.
KUJIUNGA NA KINYANG'ANYIRO CHA PIKIPIKI AINA YA BOXER BONYEZA PICHA CHINI YA MANENO HAYA NA UIBUKE MSHINDI,BONYEZA MARA NYINGI UWEZAVYO KUIBUKA MSHINDI;
Post a Comment